Saturday, September 14, 2013

KIJANA MWINGINE ACHOMWACHOMWA VISU

 Na wasamalia wema
Kijana mwingine apigwa na kuchomwachomwa visu mwilini mwake na kundi la watu maeneo ya makaburi ya don bosco barabara ndogo inayoelekea mkwawa(iringa manispaa) saa 2 usiku.kundi hili la watu lilimyang'anya simu na pesa tsh 15,000/- tarehe 12/09/2013.Hili ni tukio lingine baada ya lile la kijana aliyenyofolewa macho maeneo karibu na eneo hilihili la makaburi tarehe 08/09/2013.Sasa eneo linalozunguka makaburi haya limekuwa ni tishio kwa watu wanaopita maeneo hayo hasa wakati kuanzia saa 1 jioni na kuendelea.waliotoa taarifa hizi wanasema lengo la vibaka hawa ni vitu vidigovidogo kama pesa na simu.

No comments: